Burundi Transparence
main image
shadow shadow

 

Kambi ya Rukara au kundi la matapeli ?    Le 18 janv. 08

Serikali imeamua kuambukiza matatizo yake ndani ya jamii,hususani madhehebuni.Na dhehebu serikali imevalia njuga  siku hizi ni lile la Isilam.Katika
kukamilisha dhamira zake ,imeamua kutumia kundi dogo la waislamu ;ambao wana sifa mbaya katika jamii.Watu hawa wana nia ya kujipatia madaraka kimabavu,pasipo idhini ya waumini.Maharamiya hawa wamekuwa wakiungwa
mkono na kusaidiwa na Rais Nkurunziza.Hiyi inaonesha dhahiri kwamba Mheshimiwa Rais, hajatosheka na matatizo aliyopandikiza katika chama tawala , vile vile ndani ya chama UPRONA ,ambapo aligonga mwamba.Watu hawa wanatambulika kwamba ni walafi na wamafia.

Mmoja wao ni Burikukiye Hamza Venant, ambaye ni mwenyekiti wa shirikisho hewa liitwalo C.I.PE.B, akiwa na lengo la kusaidia yatima.Mradi huo uliungwa mkono na wafadhili wengi.Lakini kutokana na tabia yake mbaya ya kujigamba na kutumia pesa za mradi huo isivyo.Mradi huu haukuweza kufika mbali,na hivyo kujikuta akianguka katika dimbi kubwa la madeni ambayo hakufanikiwa kulipa.

Baada ya huyu mwanachama mwingine ni ; Nibaruta Mohamed El-amin, afisa mdogo  wazamani wa polisi.Huyu amepata umarufu mkubwa kutokana na utapeli wake.Vile vile ,alianzisha shirikisho ambalo limekuwa ngao ya uharamia wake.Hata misaada aliyo kupata,ilikuwa ikifikia katika akaunti yake badala ya akaunti ya shirikisho.Bila haya wala hofu alichukuwa tiketi mbili za ndege za shirika AIR BURUNDI.kwa niaba ya COMIBU , bila idhini yoyote ya mwenyekiti.Aligushi saini ya Sheikh Abubakhari Ally, mwenyekiti wa zamani wa baraza la masheikh,kwa nia ya kuchukuwa fedha kwenye akaunti isiyo kuwa yake.Bwana El-Amini alitapeli  baadhi ya watu ,akidai kwamba atawapatia viza za kwenda ulaya na Amerika.Hao ni baadhi ya wanachama wa kundi hilo,ambao hawakubaliki katika jamii ya wa islamu.

Kinara wa kundi hilo ni laana tullah Rukara Mohamed .Alitumia ‘remote control’ Rais Nkurunziza kuongoza kundi hilo kwa lengo la kusambaratisha jamii ya waislam.Watu wote hao, hawana wadhifa wowote ndani ya jammi.

Tugependa kufahamisha warundi wote, kwamba waislamu hawana matatizo na madhehebu mengine hapa nchini.Isipokwa tu chokochoko za kundi hilo na kinara
wao,ambazo zinahatarisha amani ya waislam.

Kumalizia ,tunakumbusha kwamba serikali ya Burundi haina dini ;kulingana na katiba ya nchi ambayo ilichaguliwa tarehe 28-02-2005,na kutangazwa na Raisi
tarehe 18-03-2005. Kifungo hicho cha katiba, kinakiukwa na Rais pale ambapo anaanda  mihadhara ya injili na kualika viongozi wote wa serikarili ,akitumia nyenzo za serikali, bila kusahau pesa nyingi anazo chota  kwenye akaunti ‘appui aux bonnes initiatives’Pesa hizo ni msaada kutoka Nigeria, lakini Mheshimiwa Rais anazitumia kana kwamba zake binafsi.

 

Burundi Transparence

 

horizontal bar

 

Burundi Transparence © 2007